Ayubu - Sura ya 25

Ayubu - Sura ya 25

1Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,

2Enzi na hofu zi pamoja naye; Hufanya amani katika mahali pake palipoinuka.

3Je! Majeshi yake yahesabika? Ni nani asiyetokewa na mwanga wake?

4Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu? Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?

5Tazama, hata mwezi hauangazi, Wala nyota si safi machoni pake;

6Siuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!