1Tazama, enyi watumishi wa Bwana, Mhimidini Bwana, nyote pia. Ninyi mnaosimama usiku Katika nyumba ya Bwana.
2Painulieni patakatifu mikono yenu, Na kumhimidi Bwana.
3Bwana akubariki toka Sayuni, Aliyezifanya mbingu na nchi.