Zaburi - Sura ya 136
1Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
3Mshukuruni Bwana wa mabwana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4Yeye peke yake afanya maajabu makuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7Yeye aliyefanya mianga mikubwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8Jua litawale mchana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9Mwezi na nyota zitawale usiku; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11Akawatoa Waisraeli katikati yao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14Akawavusha Israeli katikati yake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
17Yeye aliyewapiga wafalme wakuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
18Akawaua wafalme mashuhuri; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
19Sihoni, mfalme wa Waamori; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
20Na Ogu, mfalme wa Bashani; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
21Akaitoa nchi yao iwe urithi; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
22Urithi wa Israeli mtumishi wake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
23Aliyetukumbuka katika unyonge wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
24Akatuokoa na watesi wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
25Kila chenye mwili akipa chakula chake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
26Mshukuruni Mungu wa mbingu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Swahili
Italiano (it-IT)
Português do Brasil (pt-BR)
Polski (PL)
Deutsch (Deutschland)
Français (France)
Español (España)
Українська Біблія у перекладі Огієнка
English Bible - 21ST CENTURY KING JAMES (KJ21)