Zaburi - Sura ya 150
1Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.
2Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;
5Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.

Swahili
Italiano (it-IT)
Português do Brasil (pt-BR)
Polski (PL)
Deutsch (Deutschland)
Français (France)
Español (España)
Українська Біблія у перекладі Огієнка
English Bible - 21ST CENTURY KING JAMES (KJ21)