Zaburi - Sura ya 150

Zaburi - Sura ya 150

1Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.

2Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;

5Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.