Zaburi - Sura ya 61
1Ee Mungu, ukisikie kilio changu, Uyasikilize maombi yangu.
2Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo, Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.
3Kwa maana ulikuwa kimbilio langu, Ngome yenye nguvu adui asinipate.
4Nitakaa katika hema yako milele, Nitaikimbilia sitara ya mbawa zako
5Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu. Umewapa urithi wao waliogopao jina lako.
6Utaziongeza siku za mfalme, Miaka yake itakuwa kama vizazi vingi.
7Atakaa mbele za Mungu milele, Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.
8Ndivyo nitakavyoliimbia jina lako daima, Ili niondoe nadhiri zangu kila siku.

Swahili
Italiano (it-IT)
Português do Brasil (pt-BR)
Polski (PL)
Deutsch (Deutschland)
Français (France)
Español (España)
Українська Біблія у перекладі Огієнка
English Bible - 21ST CENTURY KING JAMES (KJ21)